Twitter Facebook Feed

FAIDA ZA MTI WA MWEMBE KATIKA MWILI WAKO

FAIDA ZA MTI WA MWEMBE NA MAEMBE KATIKA MWILI WAKO


Dr Hamza


Mti wa mwembe mbali ya kuzaa tunda la embe ambalo hutumika kama chakula  au kinywaji  ( juisi ) chenye ladha  ninayo  vutia, una faida  lukuki za   kiafya kwa  mwili  wa mwanadamu.

Zifuatazo  ni baadhi  ya  faida za  kiafya  za  mti  wa  mwembe.
1. MAJANI  YA MTI  WA  MWEMBE :
Majani  machanga ya  mti  wa mwembe  yakichemshwa huwa  na faida  zifuatazo  ;
i. Hutibu  pumu
ii. Hutibu kifua  kikavu
iii. Hutumika katika  kuoshea  vidonda vitokanavyo  na  majeraha  mbalimbali  (  Majani ya  maembe  yamethibitika kuwa  na  uwezo mkubwa  wa  kukausha majeraha  ya  vidonda )
iv. Unga wa  majani  ya mwembe  hutumika  katika kutunza  meno  ambapo mtu  mwenye  matatizo ya  meno  atatakiwa kusukutua  kwa  kutumia unga  unaotokana  na majani  ya  mwembe.



v. Vilevile Majani hutumika kutibia kabisa tatizo la kisukari type 2, Mgonjwa anatakiwa kuloweka majani ya kutosha kwenye maji nusu lita aache yalale huku halafu asubuhi afikiche vizuri hayo Majani kasha achue na anywe hayo maji. Anatakiwa kufanya zoezi hili kwa muda wa Mwezi Moja.

2.KOKWA LA EMBE

Unga unaotokana na  kokwa  la embe  husaidia  kuzuia kuharisha  na  kuhara damu.

3.  TUNDA LA EMBE

i.Ulaji wa  tunda  la embe  husaidia  kutibu minyoo  na  kuzuia uvujaji  wa  damu ovyo.
ii. Tunda la  embe  lina  vitamin C na  hivyo  ulaji wake  husaidia  kuponesha vidonda  kwa  haraka, hivyo basi  mlaji sana wa  tunda  la embe  endapo  atapata vidonda  basi  atapona kwa  haraka  sana kuliko  mtu  asiye tumia  tunda  hili mara  kwa  mara.
iii.  Huwasaidia watu  wenye  matatizo ya  kutokupata  choo.
iv. Utumiaji wa  maembe  mabichi husaidia  kuondoa  mawe kwenye  figo  na hivyo  kuepuka kufanyiwa upasuaji.
v.   Embe bichi  likichanganywa  na chumvi  na  sukari na  kasha  kuchemshwa   ni  tiba  ya tatizo  la  mapigo ya  moyo  kwenda kwa  haraka.
4.MAGOME YA MWEMBE



Magome  ya mti wa mwembe yakichemshwa ni dawa nzuri ya homa.

5. MIZIZI YA MWEMBE

Mizizi yake ni dawa nzuri sana kwa meno haya meno yaliyotoboka, Unachotakiwa kufanya ni kuchukua mizizi ya kutosha kasha chemsha na usukutue utwa mara 3 kwa siku 7 kwa uwezo wa Mungu utakuwa umepona kabisa tatizo la Meno.
JUISI  YA EMBE  :
Juisi  ya embe  ikichanganywa  na maziwa  fresh  husaidia kurejesha  afya  ya mtu  aliye  dhoofika.
Vile  vile kunusa  juisi ya  embe kunasaidia  kuzuia  tatizo la  kutoka  damu puani. Hivyo  basi  juisi ya  embe inaweza kutumika  kama  huduma ya  kwanza  kwa mtu  anaye  tokwa na  damu  puani.

USHAURI

Unapotengeneza Juisi ya Maembe hakikisha huweki sukari kabisa, unapoweka sukari unapunguza nguvu ya Hii Juisi katika matibabu. Vilevile unapotumia Sehemu yoyote ya Mti huu au matunda hakikisha vipo katika hali nzuri usitumie vitu vilivyooza au kuharibika.

Dr Hamza
0654729438 WhatsApp coll sms
0655729439 coll sms
Tanga Pangani Tanzania

0 comments:

Post a Comment